Privacy Policy

Last Updated: December 2025

1. Utangulizi

Asilispot Organization inajali na kulinda faragha ya taarifa zako binafsi. Sera hii inaeleza jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuhifadhi na kulinda taarifa zako unapotumia tovuti yetu, kujiandikisha kwenye mafunzo au kupata huduma zetu za malighafi.

2. Taarifa Tunazokusanya

Tunaweza kukusanya taarifa binafsi unazotupatia kwa hiari wakati wa:

  • Kusajiliwa au kuwasiliana nasi kupitia tovuti
  • Kujiandikisha kwenye mafunzo
  • Kuomba au kununua malighafi
  • Kuwasiliana na timu yetu kwa maswali au ushauri

Aina za taarifa tunazoweza kukusanya ni pamoja na:

  • Jina na mawasiliano (barua pepe, namba ya simu, anwani)
  • Taarifa za malipo (zinachakatwa na watoa huduma wa malipo kwa usalama)
  • Taarifa zinazohusiana na mafunzo (usajili, maendeleo, mapendeleo)
  • Historia ya huduma au malighafi ulizopata

3. Matumizi ya Taarifa Zako

Taarifa tunazokusanya hutumika kwa madhumuni yafuatayo:

  • Kusajili na kusimamia ushiriki wako kwenye mafunzo
  • Kutoa huduma za malighafi na ushauri
  • Kuwasiliana nawe kuhusu mafunzo, ratiba au taarifa muhimu
  • Kujibu maswali na kutoa msaada kwa wateja
  • Kuboresha tovuti, huduma na uzoefu wa mtumiaji
  • Kuzuia matumizi mabaya au udanganyifu
  • Kutimiza matakwa ya kisheria inapohitajika

4. Kushirikisha Taarifa

Asilispot Organization hauzi, haupangishi wala hausambazi taarifa zako binafsi kwa wahusika wa nje kwa madhumuni ya kibiashara.

Tunaweza kushirikisha taarifa zako pale inapobidi na:

  • Watoa huduma wa malipo ili kuhakiki malipo na kukamilisha usajili wako wa mafunzo.
  • Watoa huduma wa kiufundi wanaosaidia uendeshaji wa tovuti
  • Mamlaka za kisheria endapo itahitajika kwa mujibu wa sheria

Wahusika wote wa nje wanatakiwa kulinda usiri na usalama wa taarifa zako.

5. Usalama wa Taarifa

Tunatumia hatua za kiufundi na kiutawala kulinda taarifa zako dhidi ya:

  • Ufikiaji usioidhinishwa
  • Mabadiliko yasiyoruhusiwa
  • Upotevu au matumizi mabaya

Hata hivyo, tafadhali tambua kuwa hakuna mfumo wa mtandao au uhifadhi wa kielektroniki ulio salama kwa asilimia 100.

6. Sessions (Vipindi vya Mtumiaji)

Tovuti yetu hutumia sessions kuhifadhi taarifa za muda mfupi ili:

  • Kukuwezesha kuvinjari tovuti kwa urahisi
  • Kudumisha hali ya usajili au mawasiliano
  • Kuboresha usalama na utendaji wa tovuti

Sessions hizi hazihifadhi taarifa nyeti kwa muda mrefu na huisha kiotomatiki.

7. Cookies na Teknolojia za Ufuatiliaji

Asilispot Organization inaweza kutumia cookies na teknolojia zinazofanana ili:

  • Kuboresha uzoefu wa mtumiaji
  • Kufuatilia matumizi ya tovuti
  • Kuelewa mahitaji ya watumiaji wetu

Sessions hizi hazihifadhi taarifa nyeti kwa muda mrefu na huisha kiotomatiki.Unaweza kudhibiti au kuzima cookies kupitia mipangilio ya kivinjari chako. Sera hii itasasishwa pale matumizi ya cookies yatakapoanza kikamilifu.

8. Haki Zako

Kulingana na sheria husika, una haki ya:

  • Kuomba kuona taarifa zako binafsi
  • Kurekebisha taarifa zisizo sahihi
  • Kuomba kufutwa kwa taarifa zako
  • Kujiondoa kwenye mawasiliano ya taarifa (updates)
  • Kuondoa ridhaa yako wakati wowote

9. Faragha ya Watoto

Huduma zetu hazilengi watoto walio chini ya miaka 16. Hatukusudii kukusanya taarifa za watoto. Iwapo tutabaini taarifa kama hizo, zitafutwa mara moja.

10. Mabadiliko ya Sera Hii

Asilispot Organization inahifadhi haki ya kurekebisha Sera hii ya Faragha wakati wowote. Mabadiliko yatatangazwa kupitia tovuti yetu, na kuendelea kutumia huduma zetu kutamaanisha umekubali mabadiliko hayo.

11. Mawasiliano

Kwa maswali au maelezo zaidi kuhusu Sera hii ya Faragha, tafadhali wasiliana nasi kupitia mawasiliano rasmi yaliyopo kwenye tovuti yetu.

AsiliSpot Formulation Organization
Arusha City,
Arusha, Tanzania
Email: mawasiliano@asilispot.org
Phone: +255 768 078 727

By using our website and services, you consent to the terms of this Privacy Policy.